9 November 2014



Miss Tanzania namba mbili,ambaye sasa anachukua nafasi ya kwanza Lilian kamaziama anatatizo la kiuraia.
Hili ni kutokana na baba wa mrembo huyo jenerali kamaziama kuwa na msuguano kuhusu uraia wake,hivyo itaturudisha Kule Kule kuwa mrembo huyu Tanzania Asili yake ni mnyarwanda

"Hili Taji la mrembo wa Tanzania wahusika wangefumba macho apewe Lundenga mwenyewe tumechoka alooo"
Nimekutana na komenti hizo katika pita pita zangu leo hii katika mitandao ya kijamii nikasema wabongo shikamooni,sasa huyu mnyarwanda Yule namba tatu si ndio mrangirangi kabisa kazi ipo.
Lilian kaza buti vizuri upokee kijiti ulichoachiwa na mrembo aliyeng'atuka bi Sitti.
Ujiandae vyema na maswali ya wana habari,sio ukajijibie tu Kama upo katika vibaraza vya wapiga soga, fahamu watanzania wanakujua kuliko wewe unavyojijua yap hii ndio sifa kubwa ya wabongo kujua ya watu kuliko ya kwako kwa hiyo chunga sana.
Jus sasa watakuwa wameshafatilia vyeti vyako vya kuzaliwa ,wameshajumlisha kiwango chako cha elimu na miaka yako,wameshajua kuwa wewe sio Mtu wa Arusha,lakini ulikwenda shiriki huko na mengi mengineyo.
Usijali kuhusu uraia kwani Tanzania inamachotara kibao ha ha ha ha ha ha ha.
Kila la kheri katika kuiwakilisha Tanzania huko katika shindano la dunia.
Nimemaliza.

0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!