9 August 2014

 
Katika pitapita zangu Mitandaoni, nikiokoteza iki na kile, ghafla nikakutana na simulizi iliyovuta macho yangu, kiasi nikaona si vibaya nikaisoma na kushea na wadau, labda nao wanaweza kufaidika kwa namna moja au nyingine. Kumbuka kuwa haya ni mawazo yake mwandishi na hayana uhusiano wowote na blog ya Tmark-Turn. Kichwa cha bandiko ili kilikuwa:
Ndugu zangu sio kila kinachonga'aa ni dhahabu majuu sio mchezo, Nimekibadilisha na kuipa jina lingine Maisha Ughaibuni, ili kuvutia wasomaji wetu.

- Leo naomba mnipe nafasi nijaribu kuwasaidia baadhi ya ndugu zangu Wabongo ambao hawajafika Majuu na wanaota kufika huko, kwenda kutafuta maisha maana wanaamini kule ni Paradise.

Binafsi nilikuwa na hiyo ndoto nikaitimiza na kujionea mwenyewe na nikajifunza kwamba sio kila kinachong'aa ni dhahabu. I was once a believer of that theory kwamba Majuu ndio kila kitu mpaka nilipofika huko na kujionea mwenyewe kwa macho yangu baada ya kuishi huko miaka 30.

- Kwanza ukifika tu kama nilivyokwenda New York City/USA wabongo wenzako hata unaowajua wanakukimbia maana hawawezi kukusaidia, tatizo la kwanza makaratasi ya kukuwezesha kufanya kazi tena kazi ambazo kwenye maisha yako hapa bongo hukutegemea kuzifanya infact ni kwa mara ya kwanza nikaona Singa singa anafanya kazi kituo cha mafuta sikutegmea kuona hayo hata siku moja.

Huna makaratasi na huna pa kukaa kama umeenda kama nilivyokwenda mwenyewe kivyako vyako, itakuchukua miezi kama 6 ya kusota sana ndio uweze kupata ID na Card ili uweze kupata kazi angalau ya kulea wazee au matahira.

- So kwa mara ya kwanza katika maisha yako unakutana na kitu kinaitwa Kodi, au taxes maana hapa bongo tunacheza cheza tu na kodi kule ni serious ishu, panga pangua huwezi kupata mshahara unaozidi Dola 500 za kimarekani kwa wiki kati ya hizo watakukata angalau 100 za kodi so utabaki na 400 tu chumba 150 kwa wiki, nauli ka kwenda na kurudi kazini, halafu unagundua ili upate hgela extra ni lazima ufanye kazi masaaa mengi, so kwa mara ya kwanza unajifunza kuishi kazini maisha yako yanakuwa ni kazini tu,

- Wazungu wana akili sana System yao wameitengeza makusudi kwamba mtu kama wewe mbongo ukienda unaichangia Uchumi wao tu, uwezekano wa wewe kuwa tajiri kwa kufanya biashara kule haupo kabisa unless uuze madawa ya kulevya, ninasema tena uwezekano wa wewe mbongo kutajirika

Majuu ni haupo kabisa labda ujiunge na kuuza madawa ambayo haitachukua muda mrefu watakushika unajua kwa nini watakushika ni kwa sababu Polisi wa majuu wana akili sana wanajua kwamba hawawezi kuzuia kabisa kuuzwa madawa ya kulevya kwa sababu moja kubwa sana nayo ni Law Enforcement ya kuzuia drugs inaajiri karibu wananchi Millioni 2 wa taifa lao.

Sasa ukizuia madawa ina maana hawa hawatakuwa na kazi kwa hiyo wanavyojifanya wanazuia madawa ni waongo sana nalijua hili kutokana na kusoma Criminology nchini kwao, so wanachofanya ni kwamba kwa mfano Mjini New York.

Polisi wameugawa mji mzima kwa vipande vipande na kukata maeneo ya wauza drugs, wanaowajua one on one lakini hawawashiki hata siku kwa sharti moja tu kwamba wasiue au wasuze ile drugs ya kujipiga sindano, kwa hiyo any crime ikitokea kwenye lile eneo polisi wanamfuata muuza drugs mkubwa pale waliomkabidhi eneo ambaye siku zote ana wafanyakazi wengi mtaani kwa hiyo anajua nani amefanya anawaambia.

Polisi mara moja unashikwa, sasa wewe mbongo kwa vile hujui hii system unajiingaiza na kuanza kuuza drugs, mwenye eneo anakujua mara moja na kuwashitua Polisi ndio mwisho wako na Polisi wa Majuu hawana haraka wanaweza kukuwinda hata mwaka mzima nia na madhumuni yao kukamata system yako nzima na watakushika tu.

- Biashara ya halali huwezi kwa sababu kwanza huna capital ya kutosha na besides Wazungu wameshazoeshwa majina makubwa so siku zote wananunua kwenye maduka yenye majina makubwa, pili kodi ni kali sana huwezi kabisa maana kwenye kulipia kodi utashindwa tu so wabongo wengi majuu wanaojifanya kufanya biashara ninasema ni waongo sana always wana biashara nyingine kuliko wanayoionyesha.

- So huna choice ila kufanya kazi tu kama mbwa, ukitoka kazini ni kulala tu na kukaa ndani ya nyumba kuangalia TV hela huna mpaka mwisho wa wiki ukilipwa Wazungu wajanja sana wanakulipa kila mwisho wiki kusudi uweze kuzitumia hela zote by jumatatu ndivyo uchumi wao unavyosimama imara.

Wazungu wanajua kuwa hela wanazokulipa mshahara hazitoshi kwa hiyo wamekutengenezea system ya Credit Card yaani unapewa Card bila masharti magumu ukope, kufumba na kufumbua una madeni kuliko uwezo wako, hatimaye wanakufikisha mahali unakuwa unalipa madeni yako on interest tu bila kugusa deni lenyewe hasa deni linaendelea kuwa kubwa mpaka mwisho maisha yako ni madeni tu,

- Huku home ndugu na jamaa wanakuaminia kwamba sasa upo vizuri kumbe sio kabisa, kutuma hela huwezi wewe mwenyewe huna hela extra maana ile system haikupi hiyo nafasi, so Rafiki yako wa bongo akija unamkimbia maana huna hela extra ya kumsaidia unajificha mpaka usikie amekuwa sawa ndio unajitokeza na kujifanya kumjua sana na kwamba ulikuwa umesafiri, ndugu yako akija unamkimbia maana huwezi kumsaidia hatimaye unakata mawasiliano na home bongo maana huna pesa.

Pole pole unaanza kuwa kama Wazungu ukitembea unaongea mwenyewe kudadeki madeni yamekukaba mpaka shingoni, zamani ilikuwa rahisi ukizidiwa madeni unaenda Mahakamani una-file kufilisika wanakusamehe siku hizi hamna tena hiyo mpaka ulipe tu.

- Sasa unaanza kukumbuka bongo, hapa ulikuwa na kazi nzuri ulikuwa unaweza kula mara tatu kwa siku unaweza kwenda bar kunywa kidogo, unaweza kwenda uwanja wa Taifa kuona mipira mikubwa.

Majuu forget it it will never happen huwezi so huna pa kwenda matokeo yake mbongo mmoja akifanya party ya birthday hata ya mtoto mchanga wote mnakimbilia huko watuwazima unakuta mmejaa nyumbani kwa mbongo, kijumba kidogo mnabanana humo humo na kuanza kupiga picha za kutuma bongo kuwakoga wajinga kwamba upo majuu.

Pale kwenye party inatakiwa uwe very careful kwenye kupiga picha unatafuta angle ya kuonyesha upo kwenye bonge la nyumba kumbe mazishi matupu, umevaa nguo za kukopa dukani kwa credit card, kesho kazini mapema sana so hata pale kwenye party huna raha ila unajifanya kuwa furaha sana kumbe uongo mtupu madeni yamekukaba mpaka shingoni masikini wa Mungu,

- Matokeo yake unaanza kuja kwenye mitandao na kuanza kutukana Serikali ya Tanzania na Viongozi wake kisa na mkasa yamekushinda huko Majuu, na kurudi huwezi wengi wao wanaanza ku-develop tabia za ajabu na kutisha sana kisa maisha ni magumu na sivyo walivyotegemea lakini hawawezi kukubali na kusema wazi maana ni aibu.

Wazungu wametengeneza system yao ya maisha ili wanasheria na madakitari tu ndio wale bataz so wewe ukienda kule bila kusoma utachekesha tu, na uzuri wa Wazungu ni kwamba no matter what utakula tu maana kwa mfano usiku fast food zote wanatakiwa ikifika saa sita kutupa chakula kama kipo hakiruhusiwi kwenda next day kwa hiyo ukienda pale watakupa bure maana hawaruhusiwi kukitupa mpaka wahakikishe hakuna mtu anayekihitaji kwanza ni sheriaa.

- So unaanza pole pole kukumbuka bongo, furaha yako yote haipo tena Wazungu kama kawaida yao hawapendi weusi popote unapokwenda wewe ni nothing but nigga, huna thamani yoyote ni good for nothing halafu maisha majuu ni sheria asubuhi mpaka saa ya kulala!!!.........

OK GUYS KWA LEO NAOMBA NIISHIE HAPA NEXT NIKIWA NA TIME KAMA YA LEO WILL DO SOME MORE!!

Le Mutuz

0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!